Posts

Magonjwa yanayoongoza kusababisha vifo Tanzania

Nuzulack Dausen September 13, 2017 MWANANCHI: Mwanza/Dar. Magonjwa ya malaria, maradhi yanayoathiri mfumo wa kupumua, Ukimwi, upungufu wa damu na magonjwa ya moyo ni miongoni mwa magonjwa yaliyochangia kwa kiwango kikubwa kuchukua uhai wa Watanzania 247,976 kwa miaka 10 iliyopita katika hospitali mbalimbali hapa nchini, utafiti waonyesha. Katika ufunguzi wa warsha kuhusu sababu za vifo katika hospitali nchini iliyofanyika jijini Mwanza juzi, Mtafiti Mkuu Kiongozi wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Dk Leonard Mboera alisema lengo la utafiti huo ni kutambua ongezeko la maradhi yanayoathiri jamii. Dk Mboera alisema vifo hivyo vilitolewa taarifa kwa kipindi cha miaka 10 kati ya 2006 na 2015, huku vifo vingi vikiathiri wanaume kuliko wanawake. Alisema katika kundi la watoto chini ya miaka mitano vilichangia asilimia 20 ya vifo vyote. Utafiti Mtafiti Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR), Dk Mercy Chiduo akimuonyesha Mganga

VItu 5 hatari kwa kuua Vijana Kati ya umri wa miaka 10-19

Image
Takwimu za shirika la Afya duniani WHO zinaonyesha magonjwa ya Kuhara yameshika no.4 kwa kuua watoto walio chini ya umri wa miaka 10-19 na Huua vijana 3000 kwa Siku. Soma kurasa za chini mwa blog hii kujua namna ya kuepuka magonjwa hayo.

Wanaojisaidia kwenye chupa wabanwe

Image
MKUU wa Wilaya ya Ubungo, Kisare Makori, amesema viongozi wa masoko, mitaa na maeneo ya kazi hasa masoko wanapaswa kusimamia sheria ili kudhibiti wanaochafua mazingira kwa kujisaidia katika chupa za maji na kuzirusha katika makazi au maeneo wazi. DC Kisare alisema hayo hivi karibuni baada ya kupokea malalamiko ya wananchi waliosema baadhi ya wafanyabiashara katika Soko la Simu 2000 lililopo Ubungo Dar es Salaam, wanajisaidia haja ndogo katika chupa kisha kuzirusha katika mitalo na maeneo mengine ya wazi yakiwamo makazi ya watu na barabarani. Mkuu wa Wilaya alisema bila wafanyabiashara hao kutambua umuhimu wa usafi, kutunza mazingira na uongozi wa soko kuchukua hatua makini, ipo hatari ya kuibuka magonjwa ya mlipuko ukiwamo ugonjwa wa kipindupindu. “Viongozi wa masoko na maeneo wana wajibu wa kusimamia usafi na kuchukua hatua za kisheria kwa wanaokwenda kinyume maana kusambaza uchafu kama huo ni kosa la jinai kwa sababu mtu anayefanya hivyo anasababisha usumbufu, kero na k

Tukizingatia kufanya usafi kipindupindu kitapita mbali

Image
HIKI ni kipindi cha mvua za masika kwa karibu nchi nzima. Mvua ni baraka kwa watu, lakini wakati mwingine huwa kinyume cha baraka hizo kwani zinaweza kuambatana na athari kama mafuriko yanayosababisha uharibifu wa mali na hata kupoteza maisha ya watu. Kadhalika, mvua zisipotazamwa kwa umakini, huwa kichocheo kikubwa cha magonjwa ya mlipuko kama kipindipindu na homa ya matumbo maarufu kama taifodi. Ikumbukwe kuwa, baada ya kuingia madarakani Rais wa Awamu ya Tano, Dk. John Magufuli, alibadili shamrashamra zilizokuwa zifanyike katika sherehe za uhuru wa Tanganyika, Desemba 9, 2015 na kuzifanya zitumike kuwa kampeni ya usafi nchi nzima siku hiyo. Uamuzi wa Rais ulilenga badala ya kutumia nguvu kubwa na pesa nyingi kufanya sherehe huku eneo la afya likiwa tete kutokana na hali ya kipindupindu ilivyokuwa, Rais aliona ni busara kutumia rasilimali hizo kuzuia ugonjwa huo na mambo mengine yenye manufaa zaidi. Zuio pekee la ugonjwa wa kipindupindu ambalo ni la kisayansi ni usafi wa m

Waziri azindua kampeni ya matumizi ya vyoo

Image
Kwa ufupi Kampeni hiyo imekuja baada ya ile ya kwanza iliyoanza mwaka 2012 hadi Juni 2016 ambayo amesema ilifanikisha kuongeza uelewa katika masuala ya usafi wa mazingira. By Reginald Miruko, Mwananchi Dodoma. Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu leo amezindua kampeni mpya ya kitaifa ya usafi wa mazingira na matumizi ya vyoo mjini Dodoma iliyobatizwa “Nipo Tayari” Kampeni hiyo imekuja baada ya ile ya kwanza iliyoanza mwaka 2012 hadi Juni 2016 ambayo amesema ilifanikisha kuongeza uelewa katika masuala ya usafi wa mazingira. Amesema lengo la kampeni hiyo ni kuhakikisha mazingira yanakuwa safi na kunakuwa na matumizi ya vyoo bora kuanzia ngazi ya kaya, taasisi na maeneo ya umma. #NIPO TAYARI WEWE JE?, CHUKUA HATUA SASA.

UGONJWA WA KIPINDUPINDU (TAZAMA VIDEO)

Nchi 10 zenye mazingira safi duniani.

Image
Mazingira machafu ni miongoni mwa changamoto zinazokabili nchi nyingi duniani ambapo ongezeko la watu,sehemu za biashara na kukua kwa miji zimetajwa kama sababu kubwa inayochangia mazingira machafu hasa sehemu za mijini. April 24 2017 nimekutana na hii list ya nchi 10 zinazotajwa kuwa na mazingira masafi licha ya kuwa na idadi kubwa ya watu, list hii ni kwa mujibu wa Environmental Performance Index . Hii ni changamoto kwako ewe Mtanzania, yafanye maeneo unashoishi kuwa safi na epuka kutupa takataka hovyo: Switzerland   Switzerland ni miongoni mwa nchi zenye mazingira masafi duniani ambapo wameweza kupambana na mazingira machafu kwa zaidi ya asilimia 87.67 ,kwa mujibu wa Environmental Performance Index Switzerland ni miongoni mwa nchi zenye hewa safi. 2.  Luxembourg Environmental Performance imeipa Luxembourg asilimia 83.29  na kuifanya kuwa nchi ya pili kwa mwaka 2017 kuwa na mazingira masafi duniani. 3. Australia Australia imeshika namba tatu kwa nchi zenye mazing