Kunawa mikono, Kinga imara dhidi ya magonjwa ya tumbo na kuhara

Sababu kuu za vifo vya watoto
Shirika la afya (WHO) duniani linakadiria kwamba magonjwa ya kuhara na maambukizi ya mfumo wa upumuaji yanahusika kwa theruthi mbili ya vifo vya watoto (tazama kielelezo no 1). Shirika la umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF linakadiria kwamba ugonjwa wa kuhara peke yake huua mtoto mmoja kila baada ya sekunde30. Vifo ving vya watoto hutokea kw a watu maskini Zaidi katika nchi zeneye kipato cha kati au chini. Kwamaana hiyo Tanzania ni moja wapo kati ya nchi amabazo hupoteza watoto 2880 kwa siku na watoto 1,051,200 kwa mwaka, hii ni idadi kubwa kwa taifa.
Tanzania ni moja wapo kati ya nchi amabazo hupoteza watoto 2880 kwa siku na watoto 1,051,200 kwa mwaka, hii ni idadi kubwa kwa taifa.

                                      



                                       Kielelezo no.1  Chanzo: Shirika la Afya Duniani 2001

TUNAWEZA KUZUIA UGONJWA WA KUHARA?
Najua utakuwa umeshtushwa kwa kiasi kikubwa jinsi ugonjwa wa kuhara unavyolitafuna taifa letu. Swali ni je tunaweza kuzuia ugonjwa wa kuhara?
Jibu ni Ndio. Ugonjwa wa kuhara unazuilika na kuepukika kwa kiasi kikubwa sana. Lakini kabla hatujaangalia ni namna gani tunaweza kuepuka ugonjwa wa kuhara ni lazima kwanza tuangalie ugonjwa huu unasababishwa na nini?
Vinyesi vya binadamu ni chanzo kikuu cha vijidudu visababishavyo magonjwa ya kuhara. Vilevile ni vyanzo vya maambukizi ya shingela, homa ya matumbo, kipindupindu, pamoja na maambukizi mengine yote ya magonjwa ya tumbo na baadhi ya maambukizi ya mfumo wa upumuaji.
Inaaminika kwamba gramu moja ya kinyesi inaweza kuwa na viruisi milioni 10 na bakteria milioni 1. Vijidudu husafirishwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kama ilivyooneshwa katika kielelezo no. 2 hapo chini pia magonjwa ya kuhara na tumbo yanasambazwa kwa kiasi kikubwa na nzi, hivo watu hushauriwa kuweka mazingira salama ya vyoo, sehemu ya kupikia chakula na kufunika vyakula ili kuzuia inzi kuyafikia maeneo hayo.


                                             Kielelezo no. 2. Chanzo. Hesperian Health Guide

Najua ulikuwa na shauku kubwa ya kujua ni namna gani unaweza kujilinda mwenyewe, familia yako na jamii kwa ujumla juu ya magonjwa ya kuhara. Hizi hapa ni njia muhimu za kuepuka na kuzuia magonjwa ya kuhara:
1.      Kunawa mikono vizuri baada ya:
*      Kabla ya Kula
*      Kuwashika wanyama kama mbwa, paka, mbuzi, ngombe, nguruwe, kuku n.k
*      Kutoka chooni
2.      Kuosha matunda kabla ya kula
3.      Kuepuka kula vyakula vilivyo chacha au ambavyo havijapashwa
4.      Kuepuka kunywa maji ambayo hayajatibiwa au kuchemshwa.
5.      Kufunika vyakula vizuri baada ya kupikwa.
Utafiti wa hivi karibuni (Curtis na Cairncross, 2003) unaonesha kunawa mikono vizuri kwa sabuni baada ya kugusa kinyesi (baada ya haja kubwa na baada ya kuzoa kinyesi cha motto) kunaweza kupunguza maambukizo ya ugonjwa wa kuhara kwa asilimia 41-47.
Hivyo sabuni inaondoa kila aina ya uchafu na kuua vijidudu viliyo katika mikono.
Natumaini utakuwa umejifunza na utaifundisha jamii juu ya ugojwa wa kuhara, unaweza kushea na wengine katika mitandao ya kijamii. Kwa kufanya hivyo utakuwa umeisaidia Tanzania.




Comments

Popular posts from this blog

Nchi 10 zenye mazingira safi duniani.

Magonjwa yanayoongoza kusababisha vifo Tanzania

Maji na usafi wa Mazingira